Discuss & Debate | Share | Learn

www.ask.or.tz

Our Partners
#18813
Image

Hiki ni kitabu kilichokusudiwa kujibu yaliyochapishwa katika sehemu ya kwanza (uk. 13-42) ya kitabu cha Sheikh Juma Moh’d Al-Mazrui kiitwacho Al-Qistasu al-Mustaqim (Mezani ya Haki).

Katika kitabu hicho, Sheikh Al-Mazrui amejaribu kuthubutisha, kwa hujja alizoona zina nguvu, kwamba ile Hadith ijulikanayo kama Hadith al-Thaqalayn (Hadith ya Vizito Viwili), iliyo mashuhuri sana kwa mashia, si Hadith sahihi; ni “ya kutungwa”!

Katika kitabu hiki, Sheikh Abdilahi Nassir amezijibu hujja hizo zote - moja baada ya moja - kuthubutisha kwamba Hadith hiyo si ya kutungwa bali ni sahihi kabisa - si kwa mashia peke yao, bali hata kwa masunni.

Zaidi ya hayo Sheikh Abdilahi Nassir ameongeza sura moja humu ya kueleza, japo kwa ufupi, historia ya ukusanyaji na uandishi wa Hadithi za Mtume (s.a.w.w.), na jinsi ilivyoathiriwa na siasa na chuki walizokuwa nazo Waislamu, wao kwa wao, katika kipindi cha karne mbili za kwanza baada ya Mtume (s.a.w.w.) kufariki dunia. Amefanya hivyo ili kumsaidia msomaji aelewe vizuri kwa nini kumetokea migongano katika kuzitathmini Hadith zake.

Jina la Kitabu : Hadith Al-Thaqalayn – Hadith Sahihi
Mwandishi : Sheikh Abdilahi Nassir
Mchapishaji : Ahlul Bayt Centre

PDF Download:
http://www.shia-maktab.info/index.php/e ... ad&fid=286
Ramadhan Daily Duas- # 17

Dua for Day 17 | Holy Month of Ramadhan O Allah, […]

https://youtu.be/hk2bRbbavCY?si=6Y53rBBj5rHfPNmw

Ramadan Daily Duas - # 16

*Dua for Day 16 | Holy Month of Ramadhan* O Allah[…]

Ramadan Daily Duas - # 15

Dua for Day 15 | Holy Month of Ramadhan O Allah G[…]

Ask4help Counseling Helpline